Jumapili, 19 Aprili 2015

Vita vya kikabila:Watu 45 wauawa Nigeria

                                                     Ghasia za kikabila watu 45 wauawa Nigeria


Takriban watu 45 wameuawa kwenye mapambano ya kikabila katika jimbo la Benue, katikati mwa Nigeria.
Polisi wanasema ghasia hizo baina ya jamii za Ologba na Egba, zilizuka kutokana na umiliki wa bwawa la samaki.
Watu zaidi waliuawa pale kundi moja liliposhambulia mazishi ya mtu aliyekufa katika ghasia za awali.
Watu wengi wamelitoroka eneo hilo.
Kumetokea mapambano mengi katika jimbo la Benue katika miaka ya karibuni, lakini mara nyingi ni mizozo baina ya wafugaji na wakulima.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni