Pamoja na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuahirisha
tarehe ya kupiga kura ya maoni, Shirika la Kimataifa linaloshughulikia Elimu na
Utamaduni (UNESCO), kwa kushirikiana na Kampuni ya Focus Media pamoja na
Mtandao wa radio za jamii (COMNETA), limeamua kusambaza Katiba
inayopendekezwa kwa njia ya sauti nchi nzima, ili wananchi wapate elimu
kuhusu maudhui yaliyomo ndani ya Katiba na kufanya maamuzi sahihi pindi siku ya
kupiga kura itakapowadia.
Aidha, mkakati huo wa kusambaza Katiba inayopendekezwa
kwa njia ya sauti unajumuisha utoaji elimu kuhusu mfumo mpya wa kujiandikisha
kwa njia ya kieletroniki (Biometric Voters Registration – BVR) pamoja na
kuhamasisha wananchi ili wajitokeze kwa wingi kujiandikisha na kutimiza haki
yao ya kikatiba wakati wa upigaji kura.
Akipokea, nakala za CD zenye Katiba inayopendekezwa
kwa njia ya sauti, Mkurugenzi Mkaazi wa UNESCO nchini Tanzania Bi Zulmira
Rodrigez, alipongeza Kampuni ya Focus Media kwa kuandaa matoleo hayo na
kusisitiza radio za jamii kuzitumia ili kuwaelimisha wananchi mikoa yote juu ya
Katiba inayopendekezwa.
Mwenyekiti wa mtandao wa redio za jamii Bwana Joseph
Sekiku amewashuri watangazaji wa redio mbalimbali waliohudhuria semina hiyo
kuelimisha jamii maudhui ya Katiba inayopendekezwa ili wananchi wafanye maamuzi
sahihi katika kura ya maoni na uchaguzi mkuu.
Sekiku ameongeza kwamba kwa sasa itapatikana kupia
Focus Media pro ltd kwa kupitia mitandao yote ya kijamii na redio mtandao na
wananchi wanaweza kuwasiliana kwa kutuma ujumbe mfupi kupitia namba +255 (0)772
55 55 53
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni