Jumapili, 30 Julai 2017

RC SIMIYU;KIPAJI NI BIASHARA ,KIPAJI NI AJIRA




Mkuu wa Mkoa wa Simiyu mh Anthony Mtaka (mwenye pikipiki) akiwa katika picha ya pamoja na baadh ya washiriki wa mashindano ya mbio za Baiskeli kutoka mkoani humo ambayo yatafanyika Agosti 06, 2017 Mjini Bariadi.

Simiyu yajipanga kurasimisha kazi za sanaa, utamaduni kutengeneza ajira kwa wananchi  ambazo zitasaidia kukuza uchumi wa wananchi na Taifa kwa sambamba  kukuza utamaduni wetu.

 Aidha umekusudia kuandaa utaratibu kwa kushirikiana na wadau wengine wakiwemo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo cha Sanaa Bagamoyo na Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo kuona namna ambavyo kazi za sanaa,utamaduni na michezo zinazofanyika mkoa wa Simiyu kufanywa kibiashara ili kutanua wigo wa ajira na kuvutia watalii.


Hayo yalisemwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu Tamasha la “Simiyu Jambo Festival” litakalohusisha mashindano ya mbio za baiskeli na ngoma za asili ambalo litafanyika Agosti 06, 2017 uwanja wa halmashauri ya mji Bariadi huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa naibu spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson


Mtaka alisema vikundi vya sanaa na utamaduni vya Mkoa wa Simiyu vitapewa mafunzo ya namna ya kufanya kazi zao kitaalam na kazi zao zitarasimishwa , ziweze kuuzika ndani na nje ya mkoa ili kila mwenye kipaji atambulike.

“tunaamini Kipaji cha mtu ni biashara na kipaji ni ajira vijana wangi Mkoani hapa wanafanya vizuri katika mchezo wa baiskeli tutafanya utaratibu wa kupewa mafunzo ya kuwaimarisha zaidi katika mchezo huo, ili Mkoa ufikie hatua ya kutoa wawakilishi kwenye mashindano makubwa ya mbio za baiskeli mfano mashindano  Jumuiya ya Madola na Olimpiki”.alisema Mtaka na kuongeza kuwa:

“tungehitaji sisi kama mkoa tufike mahali ambapo kazi za sanaa na utamaduni  ndani ya mkoa wetu zifanywe kibiashara…wakati watalii wanapotembelea hifadhi za Taifa wasiishie kupiga picha na kuangalia wanyama, tungehitahiji vikundi vyetu vya sanaa na utamaduni viuze kazi zao huko”.
.
Kwa upande wake  mwenyekiti wa Chama cha baiskeli Mkoa wa Simiyu Joseph Paul amesema mashindano hayo ni chachu ya kujenga udugu, ushirikiano sambamba na kuongeza ajira huku akiishukuru  kampuni ya Jambo Food Product ya mkoani Shinyanga kudhamini mashindano hayo ya Mbio za baiskeli ambayo yatahusisha makundi matatu; kilometa 200 kwa wanaume, Kilometa 80 wanawake na Kilometa 5 kwa watu wenye Ulemavu.

“tumejipanga viziri tumeshapata zaidi ya washiriki  150 katika mikoa ya Simiyu,Geita,Mwanza, Shinyanga na Arusha na kila mshiriki lazima ajaze fomu ya ushiriki inayopatikana kwa shilingi 5000 “alisema mwenyekiti huyo

Anthony Paul ni meneja wa masoko wa kampuni ya Jambo Food  Product amesema Kampuni hiyo ambayo ni wadhamini wakuu wa Mashindano hayo wamejipanga kutoa zawadi mbalimbali ikiwemo Pikipiki itakayotolewa kwa mshindi wa Kwanza mbio za wanaume na fedha taslimu zaidi ya shilingi milioni 8 zitashindaniwa.

“mshindi wa kwanza kwa wanaume atazawadiwa pikipiki  upande wa wanawake laki tano upande wa watu wenye ulemavu shs laki mbili  na upande wa ngoma(wagika,wagalu )kila moja likipata shs milioni moja”alisema Paul
Baadhi ya Waandishi wa Habari na wadau wa michezo wakimsikiliza mkuu wa Mkoa wa Simiyu akizungumza na waandishi wa Habari juu ya “Simiyu Jambo Festival” tamasha litakalohusisha Mashindano ya Baiskeli na burudani ya wagika , wagalu na ngoma za asili Agosti 06, 2017

 
Mkoa wa Simiyu, mh Anthony Mtaka mwenye kipeperushi(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Chama cha Baiskeli, Viongozi wa Wagika na Wagalu  na baadhi ya wadau wa michezo na utamaduni mara baada ya kuzungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya Mashindano ya baiskeli yatakayofanyika Agosti 06, 2017.
Na ANITA BALINGILAKI





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni