MWENGE wa Uhuru umeanza mbio zake juzi
mkoani Simiyu na utapitia jumla ya miradi 43 yenye thamani ya shilingi bilioni 8,450,841,622
Katika kutekeleza kwa vitendo ujumbe wa
Mbio za Mwenge wa Uhuru wa mwaka
wa 2017 usemao “SHIRIKI KATIKA KUKUZA UCHUMI WA VIWANDA KWA MAENDELEO YANCHI YETU”, Mkoa wa Simiyu umetekeleza Sera ya Tanzania ya Viwanda kupitia Kauli Mbiu ya “Wilaya Moja, Bidhaa Moja, Kiwanda Kimoja”
wa 2017 usemao “SHIRIKI KATIKA KUKUZA UCHUMI WA VIWANDA KWA MAENDELEO YANCHI YETU”, Mkoa wa Simiyu umetekeleza Sera ya Tanzania ya Viwanda kupitia Kauli Mbiu ya “Wilaya Moja, Bidhaa Moja, Kiwanda Kimoja”
Aidha Mwenge wa Uhuru utafungua miradi
14, kuzindua 13, kutembelea na
kuona miradi 16 katika sekta ya Elimu,Afya,Maji, viwanda, Vijana na
wanawake,Miundombinu ya barabara, kilimo, maliasili, ushirika na utawala bora.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa mkoa wa
Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wakati akitoa salamu za Mkoa kwa Kiongozi wa mbio za
Mwenge wa Uhuru mwaka 2017 , Ndg.Amour Hamad Amour katika kijiji cha
Bukundi kilichopo wilaya Meatu ambapo mwenge umepokelewa ukitokea mkoani
singida.
“ ndani ya mkoa wa simiyu kuna viwanda
viwili maswa chaki na meatu milk ambavyo vitasaidia ajira kwa vijana huku
halmashauri zingine zikiwa kwenye upembuzi yakinifu kufanikisha ujenzi wa
viwanda”alisema Mtaka
Akifungua jengo la upasuaji kwa wanawake wajawazito
katika kituo cha Afya Bukundi wilayani Meatu kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru , Ndg.
Amour Hamad Amour ameipongeza wilaya hiyo kwa kujali afya za mama na mtoto
huku akiwataka kulitunza jengo hilo .
“miongoni mwa miradi inayogusa maisha ya
wananchi moja kwa moja, hasa akinamama wajawazito ni pamoja na huu.... nitoe wito kwa wanawake kutumia vizuri jengo
hili badala ya kujifungulia majumbani njoo hapa majumbani mnahatarisha maisha
yenu, alisema kiongozi huyo.
Mwenge wa uhuru unatarajia kupitia
halmashauri sita ambazo ni meatu, itilima, bariadi tc, bariadi dc, busega ,
maswa na july 10 utakabidhiwa mkoani shinyanga
Na ANITA BALINGILAKI SIMIYU
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni