RAIS wa Awamu ya tatu Benjamini
mkapa amewataka watanzania kujitegemea kwa kubuni miradi itakayosadia jamii kwa
lengo kuondokana na utegemezi wa mataifa tajiri.
Mkapa alisema kuwa kama taifa
tusitarajie mataifa tajiri kuja kutuinua kama sisi wenyewe tumekaa kwani ni dhana
potofu inayorudisha nyuma juhudi za maendeleo kwa wananchi.
Aliyasema hayo wakati akifungua
jengo la upasuaji katika kata ya Nkoma wilayani Itilima mkoani Simiyu ambalo
limejengwa na taasisi ya Mkapa Foundation kwa kushirikiana na nchi ya Japan .
Jengo hilo limegharimu shilingi milioni 270 ambalo litasaidia wagonjwa
hususani kina mamawajawazito kupata huduma hiyo karibu kwa awali walitembea
umbali wa kilomita 40 kufata huduma hiyo.
Aliongeza kuwa kila mtanzania ana
wajibu wa kuhakikisha taifa linajitegemea na kuwaletea wananchi wake maendeleo,
huku akiwataka wasomi na wafanyakazi kuendesha midahalo na makongamano ya
kuhakikisha nchi inajitemegea.
“ kila siku utasikia watu wanadai
haki, makongamano, midahara ya kudai haki, swali la kuwauliza wao je wametimiza
wajibu kama watanzania? Maana hakuna haki bila wajibu, ni lazima kubadilika na
kuendesha makongamano ya kuonyesha nchi itajitegemea vipi” alisema Mkapa.
Aidha ameongeza kuwa ili kuweza
kujitegemea ni lazima kila mtanzania akatimiza wajibu wa kufanya kazi kama Rais
Magufuli anavyosema, huku akitoa mfano katika nchi ya Japani kuwa wananchi wake
jambo la kwanza ni kufanya kazi.
Rais wa awamu ya Tatu Benjamini mkapa akikagua vitanda ndani ya jengo la upasuaji baada ya ufunguzi wake katika kituo cha Afya nkoma wilayani Itilima mkoani Simiyu |
“ kama tunatarajia mataifa kuja
kutuinua wakati sisi tumekaa, ni dhana potofu, viongozi tubuni miradi ili
tujiendeleze na kujiletea maendeleo sisi wenyewe, kama nchi ya Japani
wanavyofanya” alisema Mkapa.
Aliongeza kuwa toka utawala wa Baba
wa Taifa na sera ya Chama cha Mapinduzi toka zamani ilikuwa ujamaa na
kujitegemea, jambo ambalo ameeleza lazima litekelezwe kwa kila mmoja katika
kutimiza wajibu kwa nafasi yake.
Akiongelea Jengo hilo Mkapa
ameishukuru nchi ya Japana ambao walitoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo
hilo kupitia taasisi ya Mkapa foundation, huku lengo likiwa kupunguza vifo vya
akina mama wajawazito na watoto wachanga.
“ Nchi yetu bado tunakabiliwa na
changamoto ya vifo vya akina mama wajawazito pamoja na watoto wachanga, Nchi ya
Japan wametoa msaada huo kwa ajili ya kukabiliana na changamoto hii, taasisi ya
Mkapa foundation itaendeleza ushirikiano na serikali katika kutatua changamoto
mbalimbali za afya” alisema Mkapa.
Rais Mtaafu wa awamu ya tatu Benjamini Mkapa akipata maelelzo toka kwa mtaalamu wa afya jinsi kituo hicho kitakavyotoa huduma kwa wananchi mara baada ya kufungua jengo la upasuaji katika kituo cha afya nkoma wilayani itilima mkoani simiyu
Kwa upande wake mbunge wa Jimbo la
Itilima Njalu Silanga amesema kuwa pamoja na kukamilika kwa jengo hilo bado
kuna upungufu wa watumishi hivyo kuiomba serikali kuajiri watumishi ili waeze kuhudumia
wananchi.
Nao baadhi ya wananchi waliohudhuria
ufunguzi huo wamesema jengo hilo limeongeza faraja kwa akinamama wajawazito kwani
baadhi yao walikuwa wakifia njiani wakati wakisafirishwa kwenda Bariadi kupata
huduma ya upasuji.
Na ANITA
BALINGILAKI
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni