Jumamosi, 27 Mei 2017

FISI AKATISHA MAISHA YA MTOTO

                   FISI ALIYEMULA MTOTO AKIWA NDANI YA GARI LA POLISI


Hofu ilietanda kwa wakazi wa kijiji cha mwaholo kata ya mwamanenge  wilayani maswa  Mkoani Simiyu, baada ya tukio la mtoto  kushambiliwa hadi kufa na mnyama aina ya fisi kijiji hapo..

Tukio hilo ni la kwanza kutokea kijijini hapo huku baadhi ya wananchi  wakisema lina uhusiano na imani za kishirikina na wengine wakisema halina uhusiano wowote na imani hiyo.

“huyu fisi atakuwa ameasi na kufukuzwa na wenzake au yaweza kuwa ana ugonjwa maana wakufugwa haogopi watu na avizii porini” alisema mmoja wa wananchi
“haiwezekani fisi wa saa kumi na mbili bado kweupe hivi mh…kuna namna” alisema mmoja wa wanawake waliokuwa eneo la tukio

Tukio hilo limetokea juzi majira ya saa kumi na mbili jioni wakati mtoto huyo ambaye jina lake halikufahamika mara moja jinsi ya kiume (6) alipokuwa akikata kuni alizotumwa na mama yake akiwa na mwenzake  ndipo fisi alipotokea na kuwakimbiza na kumkamata mtoto huyo na kukimbia nae .  
                                                   


Mtoto aliyenusurika ambaye jina lake alikufahamika mara moja alikimbia nyumbani kutoa taarifa na jitihada za kumtafuta zilianza bila mafanikio mpaka kesho yake ndipo mwili ulipatikana ukiwa umebakizwa fuvu na mbavu.

Katika eneo la tukio baadhi ya wananchi wanasema  hali kwa sasa ni shwari kutokana na kupata msaada wa kutosha kutoka ofisi ya mkuu wa wilaya ya maswa huku wakiiomba serikali kuendelea kuwasaidia kuwasaka wanyama hao hatari wasilete madhara zaidi kwa watu na mifugo.
                                  



“ tunaishukuru ofisi ya mkuu wa wilaya kwa ushirikiano iliyotupa japo mtoto kabakizwa fuvu ila fisi kauliwa alisema mmoja wa wananchi ambaye akutaka kutaja jina lake na kuongeza kuwa nashanga mwananenge fisi wapo ila hawana historia ya kula mtu sasa huyu fisi ni fisi fisi au mtu”
                                                        



Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ambaye pia ni Mkuu wa wilaya dr self shekhalage  alisema kuwa alipata taarifa  za kuwepo kwa hali hivyo akalazimika kufika eneo la tukio sambamba na  kuitisha kikao cha kamati ya ulinzi na usalama ili kuweza kuweka mikakati ya kupambana na wanyama hao.

“tumefika eneo la tukio na kufanikiwa kumuua fisi huyo na tayari nilishatoa maelekezo ofisi ya maliasili kuhakikisha wanazunguka eneo lote kubaini kama wapo fisi wengine na kujua ni wapi walipotoka kama ni kwenye hifadhi taratibu za kuwarudisha zifanyike mara moja” alisema mkuu huyo. Na kuongeza kuwa tumesimamia mazishi ya mtoto huyo na ninawashukuru wananchi kwa ushirikiano waliouonyesha hapa.”

Hata hivyo amewataka wazazi na walezi kutowaacha watoto peke yao porini wakichunga, kucheza au kutafuta kuni ili kuwaepusha na hatari ya wanyama hao.

Na ANITA BALINGILAKI  MASWA


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni