Jumamosi, 27 Mei 2017

RC SIMIYU:TUNATARAJIA KUJENGA KIWANDA KIPYA AMBACHO AKIPO AFRIKA MASHARIKI




Mkoa wa SIMIYU unatarajia kujenga kiwanda kikubwa na chakisasa cha chaki chenye  teknolojia mpya katika Ukanda wa Afrika Mashariki ambacho kitasaidia kuongeza ajira na kukuza uchumi.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa SIMIYU, ANTHONY MTAKA katika Kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya tatu ya utekelezaji wa shughuli za Halmashauri ya MASWA na kufafanua mikakati ya mkoa katika kutekeleza azma ya serikali ya viwanda.

Tangu kuingia madarakani Serikali ya Awamu ya TANO moja ya mambo iliyoyapa kipaumbele katika utekelezaji wa ahadi zake kwa watanzania ni kuhakikisha nchi inakuwa ya viwanda na kuwa na uchumi wa kati ifikapo 2025.
Katika  kuunga mkono azma hiyo ya serikali tayari mkoa wa simiyu umeanza jitihada mbalimbali za kutekeleza azma hiyo ambayo  itatoa fursa ya ajira kwa watanzania wote.
Aidha  mh mtaka amesema kwa kuendeleza mikakati hiyo Wilaya ya MASWA tayari imeshaanza kujenga kiwanda kikubwa cha kisasa cha chaki na tayari Shilingi Milioni HAMSINI zimeshatolewa kwa ajili ya upembuzi yakinifu.
mh MTAKA ameziagiza halmashauri zote za mkoa hapa kubuni vyanzo vipya vya mapato  ili kuachana na tabia ya kuwatoza  ushuru wafanyabiashara wadogo pamoja na wakulima.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya  Wilaya ya MASWA Dokta FREDRICK SAGAMIKO amesema wameshaanza mchakato wa ujenzi wa kiwanda cha kuongeza thamani ya ngozi  chini ya ubia wa wajasiriamali wa Kijiji cha SENANI, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo -SUA na Chuo cha Teknolojia -DIT  ambacho kitakamilika Julai mwaka huu.
NA ANITA BALINGILAKI
===



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni