AMREF kwa kushirikiana na wizara ya afya maendeleo ya jamii,jinsia,wazee,na watoto wametekeleza mradi wa jenga uwezo kwa watoa huduma za afya ngazi za jamii kuongeza nguvu kwenye sekta ya afya hususan kitengo cha afya ya uzazi.
Mradi huo umetekelezwa katika mikoa mbalimbali ikiwemo
katavi na shinyanga huku mkoa wa simiyu
ukiwa wa mfano na jumla ya watendaji wa kata na vijiji 370 wamejengewa uwezo ili kusaidia kutekeleza sera kwani wao
ndo wapo karibu na wananchi awali elimu hiyo ilitolewa kwa wakurugenzi watendaji
,maafisa utumishi na wagaga wakuu wa halmashauri za wilaya zote mkoani hapo.
Akiongea kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo watendaji wa
kata na vijiji mkuu wa mkoa wa simiyu Antony Mtaka amewataka viongozi kuthibiti
ndagashida ili watoa huduma waweze kufanya kazi zao kwa umakini na kutoa
utambuilisho wa kutosha kupitia mkutano wa kijiji kuhusu ujio wa watoa huduma ili jamii iweze
kuwatambua na kutoa ushirikiano wa kutosha.
“ole wake atakayeleta habari za ndagashida atakiona cha moto
…watendaji simamieni na mtoe utambulisho wa kutosha ili ushirikiano uwepo
alisema” mkuu huyo
Mtaka amewaomba AMREF isaidie kutoa ajira kwa watu waliopata
mafunzo huku akiwaomba wadau kusaidia vifaa ili watoa huduma wanapoenda huko
wawe wamejitoleza kutoa huduma ngazi ya
jamii.
Aidha kwa upande wake dr Ama Kasangala afisa mpango wa
huduma za afya ngazi ya jamii kutoka wizara ya afya maendeleo ya
jamii,jinsia,wazee,na watoto amesema
wapo kwaajili ya kutoa elimu kuhusiana na sera ya afya hasahasa sera ya afya ya
mwaka 2014 ambayo imezungumzia afya ya msingi ngazi ya jamii .
Hata hivyo dr Kasangala ameongeza kuwa lengo la watoa huduma
ni kuzuia na sio kutibu na
watasaidia huduma za afya ndani ya familia / kaya hivyo
watakuwa kiungo kati ya jamiii na zahanati na
kupunguza msongamano wa wagonjwa.
“tunampango wa kuwafikia watu wote kwa uharaka zaidi na hasa
maeneo ambayo hayana vituo vya afya
kwa
ukaribu na ndo maana tumeongea na watendaji wa kata na vijiji wale ndo
watendaji ili watusaidie kutekeleza sera”alisema dr Kasangala
NA ANITA BALINGILAKI
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni