Jumamosi, 27 Mei 2017

CRDB BARIADI WASAIDIA KUTUNZA MAZINGIRA




Serikali wilayani bariadi mkoani simiyu kuunda sheria ndogo za uhifadhi na utunzaji wa mazingira ili kulinda uoto wa asili usipotee.
Sheria hizo zitahusisha wakata miti ovyo watupa taka ovyo hususan taka ngumu ikiwemo mifuko ya plasitiki  chupa za plasitiki na mifugo inayozurura ovyo.
Hatua hiyo ilikuja kufatia benki ya CRDB tawi la bariadi kuonyesha njia kwa kushirikiana na ofisi ya mkoa ,jeshi la polisi kuanzisha kampeni ya upandaji miti ya vivuli  kando ya barabara kuu ya bariadi lamadi,bariadi maswa .
Akiongoza zoezi hilo kamishina msaidizi mwandamizi wa jeshi la polisi Boniventura Mushongi alisema kuwa ni vema jamii ikajua umuhimu wa miti kwenye mazingira huku akisisitiza kuwa ni vema zoezi hilo likawa endelevu
“Uchumi wa bariadi unategemea kilimo na kilimo ni mvua na mvua ni uhifadhi mzuri wa mazingira hivyo basi…tukipanda miti na kuitunza mvua itanyesha sana tutalima sana na kuvuna sana” alisema Mshongi.
Mathias Mkumbo ni kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya mji bariadi  alisema  sheria hizo zitawabana wale wote wanaokiuka taratibu  za halmashauri  na  kimazingira huku akiwashukuru benki ya CRDB  tawi la bariadi na  kuahidi kutoa  ushirikiano wa kuitunza  miti hiyo .
“Tuendelee kutunza miti tutie moyo watu wanaotusaidia  ili kuendelea kuhifadhi wenzetu CRDB  wameonyesha njia upandaji miti 60 ni mfano wa kuigwa ” alisema mkumbo
Naye meneja wa CRDB Samwel Kishosha alisema kuwa lazima benki irudishe fadhira kwa jamii huku akiongeza kuwa lengo la zoezi hilo ni kufanya mazingira ya mkoa wa Simiyu kuwa na uoto wa asili  huku akitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kupanda miti katika maeneo yao ,taasisi pamoja na ofisi.

“hii itakuwa njia  mojawapo  ya  kupambana na changamoto ya ukame simiyu, mabadiliko ya tabia nchi”, alisema meneja huyo.


NA ANITA BALINGILAKI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni