Jumamosi, 9 Aprili 2016

BANGI TANI 2 ZAKAMATWA HEKARI 5 ZATEKETEZWA

Kamanda wa polisi mkoa wa Simiyu Onesmo Lyanga akiwa na baadhi ya maaskari tayari kuanza kazi ya kuteketeza bangi





Jeshi la polisi Mkoani Simiyu limefanikiwa kukamata tani 2 za bangi na kuteketeza kwa moto zaidi ya hekari 5 katika kijiji cha Ihusi kilichopo jirani na hifadhi ya Taifa ya Serengeti na pori la akiba la Maswa.
Akizungumza katika oparesheni  iliyofanyika jana katika kijiji cha ihusi Kamanda wa polisi Mkoa wa Simiyu Onesmo Lyanga alisema  kuwa  wameamua kufanya msako  huo  katika maeneo hayo  kutokana na kupata taarifa za kukithiri kwa kilimo cha bangi.
 
 bangi ikiteketezwa kwa moto
Kamanda Lyanga amesema kuwa oparesheni hiyo ni endelevu kwa mkoa huo ili kubaini vyanzo vya madawa ya kulevya na kuyateketeza kwa lengo la kuokoa kundi la vijana ambalo limeathiriwa kwa kiasi kikubwa.
Kwa upande wake    mkuu wa upelelezi mkoa wa simiyu Jonathan Shana amesema jeshi hilo limebaini mashamba zaidi ya kumi na mbili kijijini hapo hivyo oparesheni hiyo inaendelea.
           kamanda wa mkoa wa Simiyu akiwana baadhi ya maaskari kwenye moja ya shamba la bangi
Hata hivyo jeshi hilo linawashikilia watu 7 kwa kujihusisha na kilimo cha bangi  akiwemo mwenyekiti wa kijiji  kwa kushindwa kutoa taarifa yakuwepo kwa  mashamba hayo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni