![]() | ||
askari wakiimarisha ulinzi |
Tukio hilo limedumu kwa takribani saa tatu kuanzia majira ya 12:00 jioni hadi saa 20:00 usiku inadaiwa majambazi hao wapato watano walifika katika duka hilo na kumtaka mmiliki huyo wa Duka kuwapatia fedha lakini aligomba ndipo majambazi hao walimpiga risasi kifuani pamoja na mpita njia mmoja aliyefahamika kwa jina la Selemani Shaban ambapo baada ya kusikika milio ya risasi, askari polisi waliojidhatiti kwa silaha walifika eneo la tukio na kupambana kiume kuzima tukio hilo na kufanikiwa kuwauwa majambazi watatu huku wawili kati yao wakitoroka na kwamba majeruhi wote wawili waliopigwa risasi na majambazi hao, walifariki dunia wakati wakipatia matibabu katika hospitali ya wilaya ya Kahama.
Katika tukio hilo Jeshi la polisi limefanikiwa kukamata Bunduki mbili aina ya SMG na UZIGAN, magazine 3, kisu na mkanda vya kijeshi na pikipiki mbili aina san LG.
Jeshi la polisi mkoani hapa linawasaka majambazi hao ili kuwachukulia hatua za kisheria
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni