Jumamosi, 5 Machi 2016

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASWA AFARIKI DUNIA

ALIYEKUWA MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASWA BW TRANSIAS B KAGENZI ENZI ZA UHAI WAKE AKIWA OFISINI KWAKE



Waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mh Kassimu Majaliwa ameahirisha ziara yake ya kikazi  iliyokuwa ifanyike kesho wilayani maswa mkoani Simiyu.

Mh Majaliwa ameahirisha ziara hiyo kutokana na kifo cha aliyekuwa mkurugenzi mtandaji wa halmashauri ya wilaya ya Maswa bw Transis B Kagenzi aliyefariki usiku wa kuamkia leo.

Kwa mujibu wa msemaji wa halmashauri ya wilaya ya Maswa  bw Masanja Shilabu ambaye ni afisa kilimo wa wilaya  ya Maswa amesema  marehemu alikuwa akifanya mazoezi ya asubuhi  baada ya kujihisi vibaya alipelekwa hospitali ya wilaya ya Maswa.

Hata hivyo amesema kuwa baada ya hali kubadilika alipelekwa hospitali ya rufaa Bugando iliyopo jijini Mwanza kwa matibabu zaidi na umauti ulimkuta wakati akiendelea na matibabu
  
Aidha  mh Waziri mkuu anaendelea na ziara yake wilayani Meatu na kesho atahudhuria ibada ya kuuga mwili wa marehemu itakayofanyika  saa 3:00 asubuhi kwenye ukumbi mkubwa wa halmashauri ya wilaya ya Maswa,mara baada ya kuaga mwili utapelekwa wilayani Karagwe mkoani Kagera kwaajili ya mazishi

Tayari mwili wa marehemu umeshawasili wilayani maswa na kuhifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya maswa , huku taratibu za mazishi zikiendelea nyumbani kwake mtaa wa uzunguni Maswa.

"BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIIMIDIWE"

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni