Jumamosi, 30 Mei 2015

NEC YAKAMILISHA MAANDALIZI UBORESHWAJI WA DAFTARI KWA MIKOA MINNE

Maandalizi ya Kanda ya 5 Tano kati ya Sita yamekamilika jana 29/5/2015 zaidi ya BVR 1492 zinaanza kusambazwa na Tume ya Uchaguzi Kuanzia mapema Alfajiri Kanda ya Tano ni Mikoa ya Mara,Arusha,Manyara na Kilimanjaro

Jumanne, 5 Mei 2015

JAMII IMETAKIWA KUBADILIKA NA KUWATHAMINI WATU WENYE ALBINISM

Meneja wa Kituo cha Habari na Mawasiliano cha Redio Sengerema mkoani Mwanza Bw. Felician Ncheye akiwakaribisha mameneja wa Redio za jamii nchini walioshiriki kwenye mafunzo ya siku moja ya kutoa elimu kwa Redio za jamii nchini juu ya kuandaa vipindi vyenye ujumbe sahihi wa masuala yanayohusu watu wenye Albinism iliofanyika katika kituo cha Redio Jamii Sengerema hivi karibuni. Katikati ni Afisa mtetezi na ushawishi kutoka shirika linaloshughulika na watu wenye Albinism la Under The Same Sun (UTSS), Kondo Seif na kulia ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph.

Matukio ya Kisiasa Israel yakiri makosa kuhusiana na jamii ya Waethiopia

Maandamano ya Waisrael wenye asili ya Ethiopia Tel Aviv .

EAC kushughulikia mgogoro wa Burundi

Rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki mh Jakaya Kikwete