Meneja wa Kituo cha Habari na Mawasiliano cha Redio Sengerema
mkoani Mwanza Bw. Felician Ncheye akiwakaribisha mameneja wa Redio za
jamii nchini walioshiriki kwenye mafunzo ya siku moja
ya kutoa elimu kwa Redio za jamii nchini juu ya kuandaa vipindi vyenye
ujumbe sahihi wa masuala yanayohusu watu wenye Albinism iliofanyika
katika kituo cha Redio Jamii Sengerema hivi karibuni. Katikati ni Afisa
mtetezi na ushawishi kutoka shirika linaloshughulika na watu wenye
Albinism la Under The Same Sun (UTSS), Kondo Seif na kulia ni Ofisa
Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la
Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph. |