![]() |
Aliyesimama ni mgeni rasmi ambaye ni mkuu wa wilaya ya maswa dkt Self shekalaghe akiongea na waislamu kwenye baraza la Eid El Hajj |
Wakazi wa wilaya ya maswa
wanatarajia kuondokana na kero ya maji iliyoukumba wilaya hiyo kwa zaidi ya
wiki mbili kutokana na kukauka kwa bwawa la new sola ambalo lilikuwa
likitegemewa wilayani hapo.
Aidha serikali imejipanga ndani ya
wiki mbili zijazo kumaliza tatizo hilo kwa kuweka mabomba kwenye visima
ili maji yawafikie wananchi kwa ukaribu kupunguza tatizo hilo.
Bwawa hilo ndicho chanzo kikuu cha
maji katika mji huo kwenye vijiji vipatavyo 11 huku likitegemewa na wakazi
wapatao 78,190 na mifugo zaidi ya 400,000.
Hayo yalisemwa na mgeni rasmi
ambaye mkuu wa wilaya hiyo dkt self shekalaghe wakati akiongea na waislam
kwenye baraza la eid el haji lililofanyika kwenye msikiti wa baraza kuu wilaya
hapo.
“kuhusu tatizo la maji ndani ya wiki
mbili maji yatapatikana tumejipanga kuhakikisha tatizo hilo linakwisha alisema
dkt shekalaghe na kuongeza kuwa:
“jamani maji tunayoyapata sasa japo
ni meupe ila si safi na salama hivyo jitahidini kuchemsha msije pata magonjwa
ya matumbo”
Bwawa hilo ndicho chanzo kikuu cha
maji katika mji huo kwenye na vijiji vipatavyo 11 linalotegemewa na wakazi
wapatao 78,190 na mifugo zaidi ya 400,000.
Alisema moja ya sababu
zinazosababisha bwawa hilo
kukauka ni pamoja na msimu
uliopita kutokuwa na mvua za
kutosha ambazo zimechangia kwa
kiasi kikubwa hali hiyo sambamba na
baadhi ya wananchi kufanya shughuli
za kibinadamu kandokando ya eneo
la bwawa hilo na kwenye vyanzo
vinavoingiza maji katika bwawa la New
Sola.
“Mwaka jana kutokana na mvua
kutokuwa nyingi bwawa la New Sola
halikupata maji ya kutosha pamoja na
hayo lakini ukiangalia kandokando
ya bwawa na hata kwenye vyanzo vyake
vinavyoingiza maji kuna watu
wanalima mashamba,wanakata miti
hovyo na wengine hata kudiriki
kuingiza mifugo yako kunywesha
katika bwawa haya yote ndiyo
yamesababisha hali hii ya kujaa tope
na kupungua kwa kina,”
Hata hivyo ,Dkt Shekalaghe alisema
tayari hatua za dharura za zimeanza kuchukuliwa na maji yataanza
kupatikana ndani ya wiki mbili zijazo
Katika hatua nyingine amewataka waislamu wilayani hapo kudumisha umoja na amani huku viongozi wa
dini hiyo wakitakiwa kuwa waadilifu na watenda haki kwa wote
![]() |
watoto wa madrasa wakisoma QURAN kwenye baraza la Eid El Hajj |
![]() |
Baadhi ya waislamu wakiwa kwenye baraza la Eid El Hajj |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni