Jumatatu, 7 Agosti 2017

DKT TULIA AIPONGEZA SIMIYU

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Tulia Ackson akizungumza na waandishi wa habari katika mahojiano mjini Bariadi

NAIBU sipika wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk Tulia Ackson amempongeza mkuu wa mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka kwa utekelezaji wa agizo la ujenzi wa viwanda kwa asilimia 95.
Pongezi hizo zinaendana na  utekelezaji wa kauli mbiu ya  Rais wa Tanzania Dk Joseph Pombe Magufuli katika kampeni zake alipokuwa akiwaamba watanzania kuweza kumchagua ili aweze kuwatumikia kama Rais wao,lakini aliahidi kuwa moja ya vitu ambavyo anataka kuviona katika nchi ya Tanzania ni uwepo wa utitili wa viwanda katika kila mkoa .
Maneno hayo ameyasema jana alipokuwa akishiriki katika tamasha   (Simiyu jambo Festival) lililojuisha michezo mbalimbali ya asili ikiwemo uendeshaji wa baiskel kwa wanawake na wanaume nawatu wenye  uwalemavu,mgoma za asili za wagika na wagalu,michezo ya nyoka na michezo ya fisi.
Dk Tulia alisema kuwa Simiyu imekuwa miongoni mwa mikoa ya mfano katika nchi yetu kwa utekelezaji wa kauli mbiu ya Tanzania ya viwanda,kwani mpaka sasa simiyu inaviwanda zaidi ya vitano na vyote vikiwa tayari vinafanya kazi na kuongeza ajira kwa vijana wa mkoa humo.
“Nimependa kauli mbiu ya mkoa wa Simiyu isemayo wilaya moja bidhaa moja hivyo hii inamanisha ni jinsi gani mkuu wa mkoa huu alivyo na ubunifu na ushawishi wa hali ya juu kwa wananchi wake wa Simiyu” Alisema
Aidha alisema kuwa atahakikisha anakuja kujifunza kupitia mkoa wa Simiyu ili naye akafanye ya simiyu katika mkoa wake wa mbeya ili aweze kutengeneza ajira za kutosha kwa vijana wa mkoa wake kama vile ajira zilivyotengenezwa katika mkoa wa Simiyu.
Kwa niaba ya serikali tunahakikisha mkoa wa simiyu unakuwa miongoni kwa mikoa ya kipekee katika ukanda wa ziwa na hii ni kutokana na utekelezaji wa hali ya juu ya ujenzi wa viwanda.
Mbali na hilo amewapongeza wabunge wa mkoa wa simiyu kwa umoja na upendo wao katika ushirikiano wao bungeni na hata katika mkoa kwani kila mbunge wa simiyu kwenye jimbo lake kuna kiwanda hii inaonyesha ni jinsi gani wabunge na serikali wanavyoshirikiana kwa ukaribu ili kuwatumikia watanzania wa hali ya chini.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amempongeza naibu spika kwa ujio wake katika mkoa wa Simiyu na kuweza kujionea mambo mengi yaliyopo katika mkoa huo.
“Sisi kama mkoa  mbali na  kushughulika na viwanda pia tumeanza  mikakati mingine ya kuwasaidia vijana wote walio na vipaji katika mkoa huo kujisajiri”alisema mtaka na kuongeza kuwa:
“viwanda ambavyo vipo simiyu  kiwanda cha chaki Maswa,Maziwa Meatu,Busega Tomato na mazao limited,Bariadi Unga.


Na ANITA BALINGILAKI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni