Ufaulu mdogo
kwa watahiniwa wa darasa la saba mkoani Simiyu umekuwa ukisababishwa na utoro kwa baadhi ya wanafunzi na shule ya msingi igwata kwa kulitambua hilo imefanya jitihada za makusudi kikomesha tatizo hilo ili kuinua kiwango cha elimu shuleni hapo.
Hayo
yameelezwa na Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu Julius Nestory ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye
hafla fupi ya kuipongeza shule ya msingi Igwata iliyofanyika shuleni hapo.
Hafla
ilihudhuriwa na afisa elimu wa mkoa na wilaya, kaimu RPC, waratibu kata ,walimu
wakuu wa shule za msingi ,wajumbe wa kamati ya shule pamoja na baadhi ya wazazi.
![]() | |||
kushoto ni afisa limu mkoa Julius Nestory kaikati kaimu RPC Audax Selestini na kulia ni afisa elimu wa wilaya Mabeyo Bujimu |
kushoto ni mwenyekiti wa kamati ya shule Joseph Mashala katlkati ni afisa elimu mkoa Julius Nestory kulia kaimu RPC Audax Selestini
Baadhi ya wakuu wa shule ,wanakamati na wazazi
Afisa elimu huyo amesema shule hiyo ni miongoni mwa shule ambazo zimeuinua mkoa wa Simiyu kwa ufaulu mzuri kutoka katika nafasi ya 22 mwaka jana hadi kufikia nafasi ya 16 kwa mwaka 2015.
Baadhi ya wakuu wa shule ,wanakamati na wazazi
Afisa elimu huyo amesema shule hiyo ni miongoni mwa shule ambazo zimeuinua mkoa wa Simiyu kwa ufaulu mzuri kutoka katika nafasi ya 22 mwaka jana hadi kufikia nafasi ya 16 kwa mwaka 2015.
Shule ya
msingi Igwata ilikuwa ikifanya vizuri kwa miaka 7 mfululizo Mwaka huu ilishika
nafasi ya kwanza kiwilaya na kimkoa nafasi ya pili nafasi ya kwanza kimkoa ikishikiliwa na shule ya alliance iliopo wilayani bariadi huku kitaifa ikiwa ya 101.
“Ninawapongeza
sana kwa kufanya vizuri kwenye masomo yenu kwa zawadi ya gunia moja la mahindi
bado jitihada za makusudi zinahitajika.”alisema Julius
Hata hivyo
alisema Wilaya ya Maswa ina shule 120 lakini hazifanyi vizuri hivyo ni lazima
utoro mashuleni ukomeshwe.
“Nitajitahidi
kushirikiana na walimu wangu pamoja na jeshi la polisi ili tukomeshe utoro,
watoto wasome” alisema Nestory
Shule
ya msingi igwata mwaka juzi ilishika nafasi ya pili kimkoa na kitaifa
ilikuwa ya 101,mwaka jana ilikuwa ya tatu kimkoa na kitaifa ilikuwa ya
232 na ipo kilometa 70 kutoka maswa mjini.
Wanafunzi hupata uji na chakula cha mchana hali inayowafanya kutumia muda wao vizuri kujisomea badala ya kurudi nyumbani kutafuta chakula.
![]() |
wanafunzi wakipata chakula cha mchana |
Kwa upande
wa afisa elimu wa shule za msingi wa wilaya
Mabeyo Bujimu alisema walianzisha mfumo wa kuwatambua na kuwafikia
wahitimu wa 2016 kabla ya mwaka kuanza.
Naye mwalimu
mkuu wa Igwata James Mayunga alisema shule yake inafanya vizuri kila mwaka
kutokana na kamati nzuri ya shule pamoja na ushirikiano wa walimu.
Pia aliongeza
kuwa wanafunzi wanapata uji saa 4:00 asubuhi na chakula cha mchana kila siku
bila kusuasua toka mwaka mwaka 2010 ambacho kinatokana na michango ya wazazi na shule hiyo pia inamashamba.
“Utoro umepungua
kutokana na chakula tunachotoa kwa wanafunzi wetu ndio maana tunafanya vizuri kitaaluma”
alisema Mayunga.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni