Jumanne, 27 Oktoba 2015

260 WAMEFARIKI BAADA YA TETEMEKO LA ARDHI ASIA

Zaidi ya watu 260 wamefariki, kutokana na tetemeko hilo baya zaidi la ardhi, katika kipindi cha muongo mmoja.


Makundi ya uokoaji yanajikakamua kufikia maeneo ya vijijini zaidi Kaskazini mwa Pakistan na nchi jirani ya Afghanistan, ilikuwaokoa watu wanodhaniwa kuwa wameathirika na tetemeko kubwa la ardhi lililokumba eneo hilo hapo jana.
Kufikia sasa zaidi ya watu 260 wamefariki, kutokana na tetemeko hilo baya zaidi la ardhi, katika kipindi cha muongo mmoja kuwahi kukumba mataifa hayo yaliyoko bara Asia.

Image copyrightAP
Image captionMaafa makubwa zaidi yameripotiwa katika maeneo ya Kaskazini mwa Pakistan.

Zaidi ya watu elfu mbili wamejeruhiwa.
Baadhi ya maeneo yaliyoathirika zaidi nchini Afghanistan, yanadhibitiwa na wanamgambo wa Taliban, na inakuwa vigumu mno kwa maafisa wa serikali na waokoaji kuyafikia ili kutoa usaidizi.
Maafa makubwa zaidi yameripotiwa katika maeneo ya Kaskazini mwa Pakistan.

Image copyrightAFP
Image captionHali ni mbaya mno katika maeneo yenye milima na mabonde ambako kumeripotiwa maporomoko ya ardhi.

Vyombo vya dola huko vimeripoti kuwa takriban watu 214 wamepoteza maisha.
Hali ni mbaya mno katika maeneo yenye milima na mabonde ambako kumeripotiwa maporomoko ya ardhi.

Image copyrightReuters
Image captionKitovu cha tetemeko hilo lenye nguvu ya 7.5 kwenye vipimo vya Richter kilikuwa maeneo yenye milima mingi ya Hindu Kush

Aidha katika jimbo la Khyber Pakhtunkhwa utawala umetangaza kuwa watu 179 walipoteza maisha yao huku wengine 1,800 wakijeruhiwa.
Kitovu cha tetemeko hilo lenye nguvu ya 7.5 kwenye vipimo vya Richter kilikuwa maeneo yenye milima mingi ya Hindu Kush, kilomita 45 kusini magharibi mwa Jarm, Idara ya Utafiti wa Jiolojia ya Marekani imesema.

Image copyrightReuters
Image captionMajumba mengi yaliporomoka

Nchini Pakistan, vyombo vya habari vilionyesha picha za watu wakikimbia na kutoka kwenye majengo.
Bado hakuna ripoti zozote rasmi kuhusu majeruhi lakini baadhi ya ripoti zinasema watu wanne wamefariki kaskazini magharibi mwa Pakistan.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni