Jumapili, 29 Machi 2015

Raia waandamana kupinga ugaidi Tunisia



Serikali ya Tunisia inasema kuwa askari wa usalama wamemuuwa kiongozi wa kundi la wapiganaji, lilohusika na shambulio la karibuni dhidi ya makavazi katika mji mkuu, Tunis, ambapo watu zaidi ya 20 waliuwawa.
Waziri mkuu Habib Essid alisema, raia wa Algeria, kwa jina Lokman Abu Sakhra ambaye ameelezewa kuwa gaidi hatari kabisa nchini humo aliuwawa, pamoja na wapiganaji wengine wanane, kwenye shambulio lilofanywa katika jimbo la Gafsa, magharibi kwa nchi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni