Jumatano, 1 Novemba 2017

MASWA YAKOPESHA MAMILIONI VIKUNDI VYA VIJANA,WANAWAKE

wanne kutoka kulia ni mkuu wa wilaya ya maswa dkt Seif Shekalaghe na watano toka kulia ni mwenyekiti wa ccm wilaya ya maswa wakiwa kwenye picha ya pamoja na waheshimiwa  madiwani ,watendaji wa halmashauri ya maswa pamoja na wawakilishi wa vikundi vilivyopokea hundi.



Na ANITA BALINGILAKI , maswa
Jumla ya vikundi 18 jana vimepokea mkopo wa zaidi ya sh milioni 31 kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya maswa. kwaajili ya kilimo cha zao la pamba kwa msimu wa kilimo 2017/2018 .

Vikundi hivyo vimepewa mkopo huo baada ya kukidhi vigezo vya kukopesheka, jumla ya sh milioni 22,630,500 zimetolewa kwenye  vikundi 14 vya wanawake huku vikundi vinne  vya vijana vikikopeshwa sh milioni 6,556,500 na kufanya jumla  kuwa sh milioni 31,725,000

Mkopo huu utakuwa kwa kipindi kimoja cha msimu wa kilimo  wa  2017/2018  na utatozwa riba ya 10% kwa wanawake na 15% kwa vijana na vikundi hivyo vinatarajia kulima kuanzia ekari 2 mpaka ekari 51.
Wilaya ya Maswa ina jumla ya vikundi vya wanawake 323 vyenye jumla ya wanachama 6,128 na vikundi vya vijana 263 vyenye jumla ya wanachama 2,757 kati ya hao wanaume 1,810 na wanawake 947.

Awali uchambuzi wa maombi ulibaini jumla ya vikundi 205 kati ya 88 vya vijana na  117 vya wanawake vilikidhi vigezo vilivyowekwa kwenye tangazo  na baada ya uhakiki jumla ya vikundi 25 vya vijana na 31 vya wanawake vilihakikiwa hali iliyopelekea vikundi 14 vya wanawake na 4 vya vijana kukidhi vigezo vyote na kupewa mkopo.
Aidha, kwa kipindi cha miaka iliyopita (2013/2014  -2016/2017)wilaya ilitoa mkopo wa Tsh 75,955,000/=mkopo na riba kwa vikundi vya wanawake na sh 105,182,500/=mkopo na riba kwa vikundi vya vijana ,Tsh 30,162,500 mapato ya ndani na Tsh 75,020,000 zikitoka wizara ya maendeleo ya vijana habari,utamaduni na michezo.  
Akiongea kwa niada ya mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya maswa afisa maendeleo ya jamii bw lodgers lyimo amesema kuwa kipindi cha mchakato wa maombi walikutana na changamoto nyingi ikiwemo vikundi vingi vya vijana vilibainika kudanganya umri huku baadhi ya vikundi vya wanawake vikigundulika kuwa na wanaume ndani ya vikundi vyao.
Akiongea kabla ya kukabidhi hundi hiyo mwenyekiti wa ccm wilaya ya maswa Eng Paul Jidayi amesema fedha hizo zitumike kwa malengo yaliyo kusudiwa na si vinginevyo ili zilete tija na vikundi vingine vieweze kukopeshwa kupitia marejesho ya mkopo huo.
“ni vema fedha hizi zikatumike kwa kile kilichokusudiwa si tusikie mtu kanunulia vipodozi …kaongeza mke na mambo yanayoendana na hayo na kumbukeni kulipa kwa wakati ili vikundi vingine vikopeshwe”alisema  eng Jidayi
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya maswa dr Seif Shekalaghe aliyekuwa mgeni rasmi Iamesema kuwa mkopo huo umetolewa ni kwaajili ya gharama za kulimia, viuatilifu ,palizi na mbegu na utatolewa kwa awamu kwa kuzingatia hatua za kilimo.
“fedha hizo hatutatoa zote zitatoka kwa utaratibu mfano ukifika muda wa kulima mtapewa  ..muda wa palizi mpaka hatua ya mwisho na hii itasaidia kuratibu kwa ukaribu fedha hizo maana vikundi vingine vikikabidhiwa zote ni hatari” alisema dkt Shekalaghe
Mkuu wa wilaya ya maswa dkt Seif Shekalaghe  akiwa na mwenyekiti wa ccm wilaya ya maswa wakimkabidhi mmoja wa wanakikindi mbegu za pamba makabidhiano hayo yalifanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya maswa
baadhi ya watendaji wa halmashauri ya wilaya ya maswa pamoja na wawakilishi wa vikundi wakiwa ndani ya ukumbi wa halmashauri ya maswa kabla ya makabidhiano ya hundi
Mkuu wa wilaya ya maswa dkt Seif Shekalaghe  akiwa na mwenyekiti wa ccm wilaya ya maswa wakimkabidhi mmoja wa wanakikindi mbegu za pamba makabidhiano hayo yalifanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya maswa

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni