Jumatatu, 26 Juni 2017

NSSF YATOA MABILIONI MASWA



 Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama(kulia) akimkabidhi hundi ya shilingi bilioni 1.5 zilizotolewa na NSSF kama mkopo kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha chaki Maswa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt.Fredrick Sagamiko.

Shirika la taifa la hifadhi ya jamii NSSF limetoa  mkopo  wa  bilioni 1.5 kwaajili ya upanuzi wa kiwanda kikubwa ambacho teknolojia yake haipo afrika mashariki cha uzalishaji wa chaki wilayani maswa mkoani simiyu.
Mkopo huo una malengo ya kuongeza mtaji  wa upanuzi  wa uzalishaji wa chaki ambao utaleta maendeleo kwa wilaya ya maswa, mkoa na taifa kwa ujumla ,kutanua wigo wa ajira sambamba na kuongeza wanachama wa mfuko wa NSSF .
Mkuu wa mkoa wa simiyu Antony Mtaka amesema kwenye halmashauri za mkoa wa simiyu ndani ya miaka  mitano zitakuwa za  mfano kwenye halmashauri  za kipekee kwa kuwa  na miradi yake kwa kila moja mfano halmashauri ya maswa kiwanda cha chaki ,halmashauri ya meatu kiwanda cha maziwa
“Kama halmashauri tunakopa kujenga stendi kwanini tusikope kujenga viwanda vitakavyotumia malighafi zetu …vitakavyoongeza ajira na kukuza pato la halmashauri zetu na taifa kwa ujumla wake” alisema Mtaka
Akikabidhi hundi mkurugenzi  mkuu wa shirika la taifa la hifadhi   jamii NSSF  prof Godius  Kahyarara alisema mkopo huo utaendeleza adhma ya serikali ya awamu ya tano Tanzania  ya viwanda , kukuza uchumi , kuokoa fedha ambazo zilikuwa zikitumika kuagiza chaki nje ya nchi  na kuongeza wigo wa mapato  kwenye halmashauri.
“kwa vile soko kubwa la bidhaa hii  ni serikali yenyewe  mradi huu ukisimamiwa vizuri utatoa fursa  ya nchi kutumia rasilimali zake yenyewe kwa maendeleo ya wananchi  waliowengi”alisema Kahyarara na kuongeza kuwa: jambo la uweklezaji  linawezekana na lina faida na tupo bega kwa bega na serikali kwa uwekezaji wenye faida.
Kwa upande wake mgeni rasmi Waziri wa kazi,ajira,vijana,sera,bunge na wenye ulemavu Jenista Mhagama alisema mafanikio ya mradi yanahitaji ushirikiano wa kutosha kwa ngazi zote ,uadilifu ,uzalendo na weledi wa hali ya juu.
“kila mtu atekeleze kazi yake kwa uadilifu wa hali ya juu ili kuhakikisha mradi huu unakuwa na kujiendesha kwa faida na fedha yote iliyowekezwa inarudishwa kwa wakati ili kuleta faida iliyotarajiwa kwani wahenga walisema kitunze kikutunze”alisema mhagama na kuongeza kuwa:
“Baadhi ya mikoa tayari imeshachukua chaki na kuanza kuzitumia ikiwemo Zanzibar katoni 2530,  shinyanga  katoni 606, geita katoni 250, tabora katoni 100 ,mwanza katoni 50 na bado kuna oda ya kupeleka  chaki Zanzibar zenye thamani ya sh milioni mia moja arobaini”.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof.Godius Kahyarara(kushoto) akimkabidhi Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama hundi ya shilingi bilioni 1.5 zilizotolewa na NSSF kama mkopo kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha chaki Maswa, (kulia) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka.
 
 Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama( wa pili kushoto) akiangalia kikundi cha ngoma mara mara baada ya kuwasilisi wilayani Maswa, kwa ajili ya makabidhiano ya Hundi ya shilingi bilioni 1.5 zilizotolewa na NSSF kama mkopo kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha chaki Maswa.
 
 Baadhi ya viongozi katika Mkoa wa Simiyu wakifuatilia masuala mbalimbali katika hafla ya makabidhiano ya Hundi ya shilingi bilioni 1.5 zilizotolewa na NSSF kama mkopo kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha chaki Maswa.
 
Baadhi ya viongozi katika Mkoa wa Simiyu wakifuatilia masuala mbalimbali katika hafla ya makabidhiano ya Hundi ya shilingi bilioni 1.5 zilizotolewa na NSSF kama mkopo kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha chaki Maswa.

MEANDIKWA NA ANITA BALINGILAKI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni